Saturday, February 3, 2018

WAZIRI NDALICHAKO AZINDUA BODI YA USHAURI YA WAKALA WA MAENDELEO YA UONGOZI WA ELIMU

ad300
Advertisement
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako  leo amezindua bodi ya ushauri ya wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM) ambapo ameitaka bodi  hiyo iisaidie ADEM kutimiza majukumu yake ipasavyo  kwa upande wa kutoa mafunzo, nidhamu ya utendaji kazi na kusimamia vyema matumizi sahihi ya fedha zinazotolewa kwa ajili ya Taasisi hiyo.

Waziri Ndalichako ameyasema hayo leo Februari 3 Wilayani Bagamoyo mkoani Pwani na kusisitiza kuwa anategemea kuona matokeo chanya kutoka kwenye bodi hiyo kwa kuwa wote walioteuliwa wamebobea katika masuala mbalimbali yanayohusu Elimu.

Akizungumza mara baada ya maelekezo ya Waziri, Mwenyekiti wa bodi hiyo Dk.Naomi Katunzi amemhakikishia Waziri Ndalichako kuwa bodi hiyo itafanya kazi kwa kuzingatia kanuni,  taratibu na miongozo iliyopo.

Dk. Katunzi amesema kuwa wamepokea kwa mikono miwili uteuzi huo na kuwa watahakikisha wanafanya kazi kwa ushirikiano wa hali ya juu Kati ya bodi na uongozi wa ADEM.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu  Dk. Siston Masanja amesema  bodi hiyo  itaishauri  ADEM katika masuala mbalimbali ili kufikia malengo yanayokusudiwa.

Wajumbe wa bodi hiyo ni Dk. Siston Masanja ,Mick Kiliba, Dk. Eugenia Kafanabo, Dk.  Christina Raphael,  Dk. Ernest Mwasalwiba,   Gerald Mweri na  Mwanyika Semroki.

Bodi hiyo ambayo imezinduliwa leo itatekeleza majukumu yake katika kipindi cha miaka Mitatu.


Imetolewa na;

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA.

3/2/2018
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: