Tuesday, July 18, 2017

Wanasiasa 'walilia' hali ya hatari

ad300
Advertisement


Rais Joseph Kabila wa DRC

Kufuatia mapigano yaliyotokea mjini Kinshasa, mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, vyama viwili vya siasa washirika vinavyounda serikali ya nchi hiyo, vimetaka kutangazwa hali ya hatari nchini.


Imesemekana kuwa baada ya mapigano makali Ijumaa iliyopita katika soko la mjini Kinshasa, chama cha (PRPD) na chama tawala nchini humo vimetoa taarifa ya pamoja ya kutaka kutangazwa kwa hali ya hatari nchini kwa kutegemea kipengele cha 144 cha katiba. 
Katika ripoti hiyo, vyama hivyo vimesisitiza kuwa, DRC inahitaji mshikamano kwa ajili ya kupambana na kile kilichotajwa kuwa ni ugaidi.

Wakati huo huo, wapinzani wa serikali wamepinga na kukosoa suala hilo na kusema kuwa, kutangazwa hali ya hatari kuna maana ya kuzuiwa uhuru sambamba na kutoa mwanya wa kuahirishwa tarehe ya uchaguzi mkuu nchini. 

Hii ni katika hali ambayo Tume Huru ya Uchaguzi nchini humo imetangaza hivi karibuni juu ya kuwepo uwezekano wa kuahirishwa kwa tarehe ya uchaguzi mkuu nchini humo. 

Christophe Lutundula, mmoja wa wanasiasa wa upinzani na mjumbe wa kundi la vyama saba vya kisiasa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (G7), sambamba na kutangaza upinzani wake juu ya pendekezo hilo la serikali kwa ajili ya kuahirishwa uchaguzi mkuu, amesema hatua hiyo inachukuliwa kwa lengo la kutaka kumbakisha madarakani zaidi Rais Joseph Kabila.

Amesema kuwa, kuahirishwa uchaguzi, ni kinyume na katiba na hata makubaliano ya Desemba 31, mwaka 2016, yaliyofikiwa kati ya serikali na vyama vya upinzani. 

Kwa mujibu wa makubaliano hayo, Rais Joseph Kabila anatakiwa kuondoka madarakani ifikapo Desemba mwaka huu.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: