Monday, July 17, 2017

UVCCM Arusha watema cheche

ad300
Advertisement
Siku chache tangu kuibuka kwa vuguvugu la viongozi wa CHADEMA mkoani Arusha kubwanga manyanga, Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi CCM mkoa wa Arusha , umesema kauli iliyotolewa na Katibu wa CHADEMA kanda ya Kaskazini, Aman Golugwa, ikidai viongozi wa UVCCM wamewanunua madiwani wao  waliojizulu ni za uongo.

Amesema madai hayo hayana ukweli hata kidogo na kwamba UVCCM inamtaka Golugwa kuthibitisha taarifa hizo zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii  kwa ushahidi vinginevyo watachukua hatua kali dhidi yake.

Katika mkutano wa waandishi wa habari na CHADEMA uliofanyika mwishoni mwa wiki jijini Arusha, Golugwa alikaririwa akisema mjumbe wa kamati ya utekelezaji ya UVCCM mkoa wa Arusha, Joshua alimwambia kuwa "Tutawashughulikia tumekusanya fedha kutoka kwa wafanya biashara zaidi ya milioni 200."

Pia alisema kwa bahati mbaya mjumbe huyo hajui kutunza siri na kwamba amemuoa binamu yake Golugwa.

Akisoma tamko la UVCCM mkoa wa Arusha katibu wa UVCCM mkoa wa Arusha Said Goha  mbele ya kamati ya utekelezaji ya UVCCM mkoa na waandishi wa habari alisisitiza CCM ni chama kikongwe hakijahusika na hakitahusika kwa namna yeyote ile kuwarubuni wadiwani wa upinzani kujiuzulu nafasi zao na kwamba wanafanya hivyo  kwa utashi wao wenyewe.

Kwa mujibu wa Goha katika taarifa hizo wamesema taarifa za kununuliwa kwa madiwani hao Golugwa alitibitishiwa na mjumbe mmoja wa kamati ya utekelezaji ya UVCCM aliyemtaja kwa jina moja la "Mwarabu" tunaomba  wazithibitishe wa ushahidi.

Akiendelea kunukuu kauli hizo, Goha alisema CHADEMA imesema mjumbe huyo  ameoa binamu yake na katibu huyo wa CHADEMA kanda ya Kaskazini ambaye pia ni mwenyekiti wa CHADEMA mkoa.

"Tunaomba amtaje kwa jina mke huyo na uthibitisho wa cheti cha ndoa au kielelezo chochote," alisema.

Goha alisema katika maelezo yake katibu Golugwa alidai madiwani hao wamenunuliwa kwa mamilioni ya shilingi hivyo walimtaka ajitokeze ili ataje kiwango cha fedha na uthibitisho wa madiwani waliopokea fedha hizo.

Kwa mujibu wa Goha, Golugwa alisema diwani wa Ngabobo Solomon Laizer aliileza CHADEMA kuwa barua ya kujiuzulu hakuandika yeye wala sahihi iliyoko kwenye barua hiyo siyo ya kwake.

"UVCCM tunamuomba diwani huyo ajitokeze hadharani kuthibitisha au kukanusha kauli hiyo," alisema.

Aidha, UVCCM umeitaka CHADEMA kutambua kuwa CCM ni chama kikongwe kimepitia kwenye misukosuko mingi  na bado kipo imara hakiwezi kutetereka na kwamba madiwani waliokuwa wa CHADEMA wakajiuzulu hata wangeendelea kubaki CHADEMA hawaizuii serikali ya CCM kuendelea kutekeleza ilani yake.

"Niwakumbushe tu CHADEMA kuwa mwenyekiti wao wa taifa  Freeman Mbowe hivi karibuni alisema kuwa katika uchaguzi mkuu wa 2015 walifungua milango na madirisha na kuacha kila aina ya mdudu kuingia, sasa wanaotoka wasiituhumu CCM kwa kutafuta mchawi watambue wachawi ni wao wenyewe," alijinasibu.

Aidha alitumia fursa hiyo kuitaka CHADEMA kuangalia walipojikwaa badala ya kuangalia walipoanguka.

Pamoja na hayo, aliitaka CHADEMA kujiuliza kama wanachama wa chama hicho kwa mikoa mingine wanaohamia CCM kama wamenunuliwa pia kama anavyoodai ama lah. 

"Au tuwaulize CHADEMA mawaziri wakuu wastaafu Fredrick Sumaye na Edward Lowassa na mzee Kingunge na wengine wengi CHADEMA imewanunua kwa shilingi ngapi?" alihoji.

Shechambo blog ilipomtafuta Golugwa kwa simu, jitihada ziligonga mwamba baada ya simu yake kutokuwa hewani kwa muda mrefu mpaka habari hii inakamilika kuandikwa.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: