Sunday, August 31, 2014

Mfumo mpya wa GPA 'kuwahukumu' wanafunzi

ad300
Advertisement
BARAZA la Mitihani la Taifa (NECTA), limesema litaanza kutumia mfumo wa wastani wa pointi (GPA) katika upangaji wa ufaulu kwa watahiniwa wa kidato cha nne na sita.

Hatua ya kutumika viwango hivyo ilifikiwa na Bodi ya NECTA katika mkutano wa 98 na tayari serikali imeridhia kutokana na kuonekana kuwa na viwango.

Kuanza kutumika kwa mfumo huo, kutasaidia kukuza kiwango cha elimu na kuondoa malalamiko kutoka kwa wadau wa elimu wakiwemo wanafunzi.

Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk. Charles Msonda, alisema juzi mjini Dar es Salaam, kuwa mfumo huo ni rahisi kueleweka na utasaidia kupunguza malalamiko kuhusiana na viwango vya ufaulu.

Alisema katika upangaji wa matokeo ya mtahiniwa mfumo wa GPA utatoa tafsiri itakayoonyesha kuwa mwenye GPA kubwa ndiye aliyepata matokeo mazuri na mwenye GPA ndogo ndiye aliyekuwa na ufaulu wa chini.
"Utaratibu wa kuandika GPA huandikwa katika nafasi moja ya desimali na nafasi ya pili ya desimali hukadiriwa katika makumi ya karibu," alisema huku akitolea mfano wa GPA ya 3.15 kuwa sawa na 3.2 na GPA ya 3.14 kuwa sawa na 3.1.
Alisisitiza katika mfumo wa makundi alama ya juu ya ufaulu itaanzia A 75-76 ambayo ni bora sana, B+ 60-74, Vizuri sana, B 50-59 Vizuri, C 40-49 Wastani, D 30-39 Inaridhisha, na F 0-19 ambayo ni feli.

Aliongeza kuwa mtahiniwa aliyepata daraja la kwanza la pointi saba kwenye mfumo wa jumla ya pointi, atapewa daraja la ufaulu bora sana (Distinction) kwa wastani wa pointi 5.0 pindi ukokotoaji wa madaraja ya ufaulu utafanyika kwa kutumia mfumo wa wastani.

Dk. Msonde alisema baada ya mabadiliko hayo wameshirikiana na wadau mbalimbali katika kuhakikisha ufanisi zaidi katika mfumo huo.

Pia, wameanza kusambaza elimu kwa wadau kuhusiana na mfumo huo.

Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: