Friday, April 13, 2018

Utaratibu mzuri wa kuendesha gari ya 'Automatic gear'

ad300
Advertisement
KWA dereva yeyote, ni wazi hawezi kupingana na mimi kwamba gia ni eneo muhimu sana kwenye gari ambalo limeundwa kwa makusudi ya kutoka sehemu moja kwenda nyingine yaani kuwa na mwendo.

Gia ndio inayofanya gari itembee kwa mwendokasi mkali au mdogo kadri dereva atakavyoamua kufuatia ubadilishaji wake wa gia akiwa kwenye mwendo.

Kitendo cha kubadili gia, kutokana na utafiti wa kitaalamu kwa baadhi ya madereva kilionekana kuwa changamoto ambapo wengi walionekana kuiumiza gari kwa kutembelea gia ambayo haikustahili kutumika kwa eneo na wakati husika.

Ni kutokana na majibu hayo ya utafiti na maendeleo ya sayansi na teknolojia wataalamu waliona badala ya kumpa shida dereva kubadili gia mara anapokuwa akiendesha gari wakaamua kuunda mfumo wa gia ambao gia zinajibadilisha zenyewe yaani automatic driving.

Kimsingi katika gari za AUTOMATIC kuna gia ambayo ina alama zinazosomeka L, 2, 3 na O/D.

Napenda ufahamu  kuwa katika hali ya kawaida wakati unaendesha gari yako inapaswa kuwa katika gia ‘’D’’ kwa maana ya ‘’DRIVE’’ na hii inategemeana na mazingira ya barabara na kama kuna hali yali ya hewa nzuri.

Gia 2 na 3 hutumika tu pale unapokuwa ama unashuka au unapanda mlima/mteremko mkali sana na mrefu mfano Sekenke, Wami au Kitonga na unataka ushuke au upande kwa spidi ile ile ila isizidi 40/60.

Namba 2,3 na L kwenye gia yako inamaana kuwa ina inazuia 'gear box' ili gia zisibadilike (-/+) kama ambavyo zinabadilika ukiweka D na itambulike kuwa unaweza kubadili kutoka D kwenda 2 au 3 wakati wowote gari inapokuwa katika mwendo.

Hata hivyo kuna tahadhari kwamba ukitaka kufanya hivyo, hakikisha usiwe spidi zaidi ya 60, kwa sababu kinachofanyika ni kwamba D inasababisha sahani (disks) zilizomo ndani ya 'gear box' kufanya kazi na hii husababisha ile hydrolic 'mafuta ya kulainisha gia' yaliyomo ndani kupata joto.

Joto hilo hutoka katika zile sahani ambapo mwisho wake joto lile husababisha gear box kutokuwa na nguvu ile ile (constant velocity) na ndio maana ukiweka namba 2, 3 au L, gear box inakuwa kwenye 'lock' na sahani hazisuguani kwa sababu inakuwa inatumika sahani/disk moja tu kwa hiyo inasaidia ile hydrolic kupoa na kufanya gari iongeze nguvu kwa ghafla.

Gia L inatumika pale unapokuwa ama umekwama au unavuta gari jingine ila inapaswa itumike kwa muda mfupi sana maana ina nguvu kupita kiasi na pia inaongeza ulaji wa mafuta.

Hivyo kama ukitoka katika mkwamo na unaona bado barabara si nzuri  labda ina utelezi au unavuta mzigo kwa mwendo mrefu basi unaweka 2 au 3 na wakati huo huo unaweza kuweka hata D kama hali ya njia na mzigo vinaruhusu.

Ukiwa katika hali hiyo unaweza kuongeza walau mpaka spidi 60 au zaidi kama utaweka D kwa maana rahisi zaidi kwamba gia namba 2,3 na L zinafanya kazi kama gari ya Manual nikimaanisha ile isiyo ya automatic na hii inakuwa rahisi kwa yeyote ambaye anafahamu kuendesha manual.

OVER DRIVE (OD) inatumika pale gari inapokuwa spidi zaidi ya 60/80 kutegemea na aina ya gari na hili hutokea bila wewe kujua maana gari yenyewe ndo inafanya ndio maana unashauriwa iwe ON muda wote kusudi gari ichague ni wakati gani iweke ON au OFF.

Kumbuka ukiwa chini ya spidi 60 hata kama umeweka ON bado inakuwa haifanyi kazi, ndivyo walivyoiunda wataalamu na hayo ndio maajabu ya teknolojia tunayoyazungumzia.

OD unaweza kuitumia kama breki ya ghafla au stop engine hasa unapokuwa zaidi ya spidi 80 na wakati huo iko ON yaani katika dashboard taa ya OD unapaswa kuwa imezima kwa sababu ikiwaka maana yake iko OFF, ukiona hivyo basi ili upunguze mwendo kwa haraka unachofanya ni kuweka OFF na wakati huo unakanyaga breki taratibu.

Kwa kitendo hicho ambacho kinatakiwa kuwa cha haraka utaona gari linavyopunguza mwendo taratibu na wakati mwingine si lazima ukanyage breki, iweke OFF halafu toa mguu katika pedali ya mafuta gari lazima ipunguze mwendo yenyewe na kama ilikuwa ni tuta na umeshalipita basi iweke tena ON, ongeza mafuta au unaweza kuweka 2 au 3 ili gari ianze kwa kasi zaidi.

Baada ya  kuchanganya basi rudi kwenye D na endelea kama kawaida na kuliongoza gari lako kwa umakini na usalama wa hali ya juu.

Tahadhari

Kamwe usikate kona wakati uko spidi kubwa na gia namba tano (MANUAL) au rpm iko 3000 (AUTOMATIC), hii husababisha kupitiliza au gari kuanguia kwa sababu katika hali hii gari inakuwa nyepesi sana.

Hakikisha umepunguza mwendo mpaka gia namba nne na kanyaga breki kidogo kama unatumia gari yenye mfumo wa manual ambao unakukazimu ufanye kila kitu ikiwemo kubadili gia na Kwa AUTOMATIC weka gia namba  2 au 3 ila lazima OD iwe OFF na uwe umekanyaga breki kidogo.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: