Friday, April 13, 2018

Simu inasababisha saratani?

ad300
Advertisement
"Usiweke simu karibu na unapolaza kichwa chako usiku, ni hatari kuna mionzi itazuru ubongo wako na utapata saratani ya ubongo, ukipata meseji hii mtaarifa na umpendaye... Mimi nimeanza na wewe!

Niambie, umewahi kupata ujumbe wa namna hii kwenye simu yako ya mkononi tena kwa mtu unayemjua kabisa anaweza kuwa ndugu, rafiki au hata jirani? Bila shaka jibu litakuwa ndio kuonyesha kukubali na inawezekana nikikupa nafasi ya kujieleza ukaniambia "Si mara moja."

Hizi kimsingi ni baadhi ya jumbe ambazo watumiaji wa simu za mkononi huzisambaza kwa mtu au watu kwa mfumo maarufu unaoitwa "Copy & Paste" kwa sababu ameipokea kwa mtu A akaona una manufaa japo hajiulizi kama una ukweli wowote au lah, yeye huamua tu kutuma kwa mtu B au mara zingine mtu C, D na hata F.

Jumbe hizi huleta hofu kwa mwingine, licha ya kwamba mtumaji alikuwa na nia njema lakini haweza kufanya aliyepokea akaanza kuiogopa simu yake kwa kigezo tu cha kuwa mbali na majanga ya kupata saratani ya ubongo.

Ni wazi kuna aina lukuki za saratani kwa miaka ya hivi karibuni ikilinganishwa na miaka 50 iliyopita na ukweli ni kwamba saratani yoyote ile inatisha kwa sababu kwa mujibu wa madaktari na wataalamu wengine wa utafiti wa afya za binadamu, bado haina tiba, mionzi hufanya kwa kiasi tu japo watu hupona kwa imani za kiroho.

Hoja ya simu za mkononi kusababisha saratani kutokana na madai kuwa zina mionzi mikali inayodhuru ubongo wa binadamu ni ya muda mrefu, sijaona utafiti wowote uliofanyika kufikia muafaka huo kwa sababu nimepekua maeneo mengi bila mafanikio zaidi ya kupata majibu ya tafiti zinazoangalia kuhusu kukanusha madai hayo.

Kwa maana hiyo utafiti upo, hata kama ulifanywa kwa kiwango kidogo au sampuli ndogo, kwa kitendo cha mimi kuona tu utafiti huu mpya naamini wapo watu walichunguza na kubaini ukweli kuwa simu za mkononi husababisha saratani; kwani utafiti hupingwa na utafiti huu ndio ukweli.

Utafiti huu niliouona imefanywa na kusimamiwa na Shirika la Marekani linalosimamia Chakula na Dawa FDA, (ambayo ni taasisi kama ilivyo TFDA hapa nchini) kwa kushirikiana na Mpango wa kitaifa nchini humo unaohusika na masuala yanayohusu sumu (National Toxicology Program).

Kwa maelezo yao, simu ya mkononi ili kuweza kuwasiliana na mtandao wa mawasiliano kuna miyonzi ambayo inakuwa inatoa au kuzalisha mionzi inayojulikana kama Radiofrequency.

Mionzi hii inatajwa kuwa haina ukali mkubwa kama mionzi inayotolewa na vipimo vya X-ray ambavyo vinatoa mionzi inayotambulika kama ionizing yenye uwezo wa kupenya nyama na kufikia mifupa ya mwanadamu huku ikiua baadhi ya seli.

Wataalamu wa afya wanasema vifo hivi vya seli ndivyo kitaalamu husababisha saratani pale ambapo vitendo vya tiba vinapotoa mrejesho hasi.

Nini kilifanyika?

Kwenye utafiti huo kundi la panya liliwekwa kwenye mazingira yaliyozungukwa na mionzi ya radiofrequency muda wote na kiwango cha mionzi hiyo kiliwekwa juu kuzidi hali ya kawaida ya mionzi inayotolewa na simu tunazozitumia.

Moja ya matokeo ya utafiti huo yalionesha panya wa kiume ndio waliathirika zaidi, ambapo walipata uvimbe fulani ulioanza kukua maeneo ya mioyo yao.

Panya wa kike ambao pia walikuwa kwenye eneo hilo hilo hawakupata madhara yoyote hasi yaliyoonekana na wataalamu hao lakini jibu la mwisho likawa uvimbe kwenye mioyo ya panya dume haikuwa aina yoyote ya saratani.

Wataalamu hao walikwenda mbali zaidi ya utafiti wao kwa kuwafuatilia kwa ukaribu panya wote baada ya kukamilisha utafiti wao ambapo walibaini wale ambao walikuwa kama sampuli ya utafiti waliishi umri mrefu zaidi ikilinganishwa na jamii ile ile kwa ambao hawakuguswa kabisa na jaribio hilo la kitaalamu. Hawakutoa majibu kwanini hali hii ilitokea!

Tunafahamu kwamba kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia kuna mifumo mbalimbali ya mawasiliano ya simu ikiwemo 2 generation au kwa kifupi 2G (Edge), 3G, 4G na kwa wenzetu walioendelea wameshafika 5G sasa panya hao waliwekwa kwenye eneo lililofungiwa kiwango cha juu cha mionzi ya radiofrequency katika mfumo wa 2G na 3G.
Waliishi kwenye eneo hilo kwa muda wa miaka miwili ambayo kwa makadirio ya kitaalamu umri wa miaka miwili wa panya ni takribani miaka 70 ya mwanadamu.

Angalizo walilolitoa wataalamu wale ni kwamba "Matokeo ya utafiti huo yasihusishwe moja kwa moja na madhara yanayoweza kutokea kwa utumiaji wa simu wa mwanadamu kwa sababu panya hao waliwekwa kwenye kiwango cha juu sana cha mionzi kuliko kiwango cha kawaida kinachotolewa na simu."

Kiuhalisia ni sentensi niliyoitafsiri kwa ufasaha kabisa kutoka lugha ya kiingereza kuja kiswahili lakini bado inaonekana kuwa ngumu kueleweka, si ndio? Sasa akili kichwani mwako, bora nusu shari kuliko shari kamili kwa sababu nilizungumza jana kwenye safu hii hii kuwa matumizi yoyote ya kitu chochote ni hatari hivyo tutumie vifaa hivi kwa kiasi.

Utafiti huu kwa ufupi umebainisha hakuna madhara ya kiafya kwa watumia simu, lakini wanaweza kuja watafiti wengine wakasema utafiti wao umebaini kuna madhara makubwa tena sana kiafya kwenye matumizi ya simu, chonde chonde nisionekane muongo katika hili.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: