Friday, April 13, 2018

DART yasema ina muarobaini wa 'mafuriko' Jangwani

ad300
Advertisement

KAMPUNI ya mradi wa Mabasi yaendayo Haraka (DART), imesema ipo mbioni kutafuta muarobaini wa tatizo la mafuriko kwenye karakana yake ya Jangwani, Dar es Salaam.

Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Mtendaji Mkuu wa DART, Mhandisi Ronald Lwakatare, alipozungumza na gazeti la Uhuru ofisini kwake.

Lwakatare alisema wakati wanajenga karakana hiyo, walichukuwa tahathari ili kama yakitokea mafuriko yasiweze kuharibu miundombinu hiyo iliyogharimu serikali fedha nyingi.

Alitoa kauli hiyo, katika wakati ambao gazeti la Uhuru limeshuhudia maji yakiwa tatizo kwenye eneo ilipo karakana hiyo, kila unapotokea msimu wa mvua.

“Serikali ipo mbioni kutafuta ufumbuzi wa tatizo lililopo katika karakana ya Jangwani na tunazo njia mbadala za kufanya kwenye usanifu ili kupata ufumbuzi wa kudumu wa tatizo hili,” alisema Lwakatare.

Pia alisema licha ya kwamba mvua za misimu ya mvua huleta athari katika karakana hiyo, bado haijahamishwa kama taarifa kadhaa za upotoshaji zilivyodai na kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii nchini.

“Shughuli za DART zinaendelea kama kawaida kwenye karakana yetu ya Jangwani,” alisisitiza.

Kuhusu mwendelezo wa ujenzi wa barabara ya mabasi yaendayo kasi Dar es Salaam (BRT), kutoka Kamata, Kariakoo mpaka Mbagala, Mtendaji huyo alisema, ujenzi wake bado haujaanza lakini unatarajiwa kuanza muda wowote ndani ya mwaka huu.

Imeandikwa na Hamida Said

Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: