Thursday, April 12, 2018

Ben Pol kuja kivingine

ad300
Advertisement
NYOTA wa muziki wa Bongo Fleva, Bernard Poul  ‘Ben Pol’ ametoa wimbo wake mpya uitwao ‘Napenda nipate lau nafasi’ ambao umekuwa gumzo kutokana na staili aliimba.

Wimbo huo, kwa mara ya kwanza uliimbwa na mwanamuziki Marijani Rashid, akiwa na bendi ya Kilwa Jazz na kufanya vizuri zaidi katika stesheni mbalimbali za redio na televisheni nchini.

Ben Pol ambaye anatamba na nyimbo mbalimbali zikiwemo ‘Sophia’, ‘Natuliza bolli’ , ‘Jikubali’ na nyingine nyingi ambazo zinafanya vizuri kwenye vituo mbalimbali vya televisheni na redio.

Ben Pol kwa kushirikiana na msanii mwenzake Wyse wameamua kuurudia wimbo huo kutokana na mapenzi na waimbaji wa bendi ya Kilwa Jazz.

“Mara nyingi muziki wa bendi unavutia na unaujumbe mzuri, wengi waliotangulia kufanya muziki huo walifanya vizuri hivyo nimevutiwa na wimbo wa Jazz Band Napenda lau nipate nafasi kwa sababu ni nyimbo ambayo nikipenda sana kuisikiliza hapo nyuma,” amesema Ben Pol.

Ben Pol amesema marehemu Marijani na bendi zingine ikiwemo Sikinde, Moro Jazz,Tanka Talamasi na Tabora Jazz ni miongoni mwa bendi ambazo zinamfanya atamani kufanya muziki mzuri na pia kujifunza zaidi kupitia nyimbo zao .

Amesema anayefanya kazi mzuri siku zote hukumbukwa kwa jitihada na uwezo wake hivyo nyimbo hizo zitaendelea kuwa mfano wa kuigwa na wengi ambao wanapenda kujifunza au kufanya muziki wa aina hiyo.

Kufuatia uamuzi wa Ben Pol kuurudia wimbo huo huku akiuongezea vionjo, wapenzi wa muziki huo nchini wamepongeza kazi hiyo huku wakisema ameutendea haki.

Habari hii imeandikwa na Mwanaheri Masoud
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: