Monday, August 28, 2017

Wasomi watakiwa kujitathmini upya

ad300
Advertisement
Wanataaluma katika fani mbalimbali hapa nchini wametakiwa kutojivunia usomi na maarifa waliyopata na badala yake wafanye kazi ili kusaidia jamii inayowazunguka kuondokana na changamoto mbalimbali.

Hayo yalisemwa na Mwanazuoni wa Kiswahili, Profesa Tigiti Sengo (pichani aliyesimama), wakati wa hafla ya kukumbuka uzoefu na mchango wake katika taaluma na hususani katika lugha ya Kiswahili iliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Dar es Salaam.

Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na wadau wa lugha kutoka ndani na nje ya Tanzania, Profesa Sengo alisema wakati umefika kwa wasomi mbalimbali kufanya tafiti zitakazotoa majibu ya changamoto mbalimbali katika Jamii badala ya kujisifu.

“Kuna umuhimu wa wasomi na watafiti kufanya tafiti katika masuala mbalimbali kama dini na dhana zake ili kuisaidia Jamii badala ya kuacha watu wakipotoka,” alisema.

Pia alisema ni muhimu kwa jamii kufahamu kuwa changamoto ni sehemu ya maisha hivyo kutafuta majawabu na kujenga mazingira ya kutetea haki bila woga.

Kwa upande wake, Profesa Abdala Safari, ambaye ni mwandishi wa vitabu alisema maisha ya Profesa Sengo ni mfano wa kuigwa na wasomi wa Tanzania kwa kuwa ametumia muda mwingi kujibu changamoto mbalimbali za Jamii kwa kuwasaidia kupata mahitaji yao.

“Wasomi wana wajibu mkubwa wa kutumia muda wao kusaidia jamii kwa kutoa ushauri ili Jamii itekeleze yatakayosaidia kuinua Jamii husika kimaendeleo,” alisema Profesa Safari.

Aidha aliwataka wasomi kuandika vitabu na matini mbalimbali vitakavyosaidia Jamii kupata maarifa na ujuzi kama mbinu ya kumuenzi Profesa Sengo.

Said Masomaso, Mhadhiri katika Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), Chuo Kikuu Huria cha Tanzania alisema kuwa Profesa Sengo ametoa mchango mkubwa katika kutafsiri maneno mbalimbali ya kisayansi na teknolojia katika lugha ya Kiswahili.

“Naishauri serikali kuendelea kuwasaidia wazee kama hawa kwani wana mchango mkubwa katika Jamii,” alisema Said.

Profesa Tigiti Sengo ni mhadhiri mwandamizi ambaye amewahi kuhudumu katika vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini na nje ya nchi na ameandika zaidi ya vitabu sitini, machapisho na matini zadi ya 100 katika lugha ya Kiswahili ambayo yanasaidia jamii kupata maarifa katika mada mbalimbali za lugha, fasihi, na sarufi.

Imeandikwa na Vincent Mpepo, OUT
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: