Tuesday, August 29, 2017

RC Gambo acharuka migogoro ya ardhi isiyokwisha

ad300
Advertisement
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo, amesema waandishi wa umma katika kata mbalimbali za jiji la Arusha na gharama kubwa za upimaji wa ardhi ni baadhi ya sababu za migogoro mingi ya ardhi inawafanya wasio na uwezo kushindwa kumiliki ardhi. 

Aidha aliwanyooshea kidole wanasiasa pamoja na watendaji wa kata kwakua sehemu ya migogoro hiyo kwa maslahi yao binafsi ya kisiasa badala ya kujali maslahi ya wananchi wanaowaongoza katika maeneo yao.

RC Gambo alisema watu hao wamekuwa wakipenda pesa zaidi kuliko kusimamia utu na haki za wananchi ambapo aliagiza kila halmashauri za mkoa wa Arusha kuhakikisha wanaweka taarifa za walalamikaji wa migogoro ya ardhi ili malalamiko hayo yashughulikiwe na kupatiwa ufumbuzi. 

Aliyasema hayo leo Agosti 29, kwenye kikao chake na wataalamu wa Ardhi,Viongozi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Idara ya Uhamiaji, Polisi, Watendaji wa Kata na wananchi wenye kero mbalimbali za ardhi jijini Arusha ili kuzisikiliza na kuzitatua. 

Katika kikao hicho kilichofanyika katika ofisi za jiji la Arusha, alisema migogoro mingi ya ardhi inasababishwa na gharama kubwa za upimaji ardhi ambazo wananchi hawazimudu jambo ambalo alisema linapaswa kuangaliwa upya na kuweka gharama rafiki kwa wananchi na kuwawezesha kumiliki ardhi.

Pia alionya wanasiasa kuacha mara moja tabia ya kutumia kero za wananchi kama mtaji wao wa kisiasa kwakua kwakufanya hivyo hawaijengi jamii wanayoingoza Katika kuzipatia ufumbuzi kero zao bali malumbano yasiyo na tija.

Akizungumzia watendaji wa kata, alisema wapo katika kata hizo kwaajili ya kusogeza huduma bora za kiserikali kwa wananchi na pale kero inapowashinda wanapaswa kuiwasilisha ngazi za juu yao badala ya kuitumia migogoro hiyo kujipatia fedha huku migogoro ikiendeleakuwatafuna wananchi.

Kuhusu waandishi wa umma aliwataka kuwaandikia wananchi mikataba isiyo na utata kwa lengo la kujali fedha zaidi kwani baada ya wao kupata fedha zao kinachofuata ni kuwaaachia wananchi waliouziana maeneo migogoro isiyokwisha.

Aidha alikemea tabia ya nakala za hukumu za mashauri ya ardhi kucheleweshwa kutolewa halia mbyo inasababisha wale wananchi wanyonge ambo wameshinda katika kesi zao kukosa ushahidi na kuzidiwa nguvu na wale wenye fedha na ardhi zao kuchukuliwa.

Hili suala ni lazima sasa tulichukue kwa uzito wa pekee haiwezekani watu wanakero za ardhi tangu mwaka 1989 hadi leo hii inamaana hakuna viongozi wanaoshughulikia suala hili, inasikitisha hapa kunarushwa ndani yake, kwanini watu walalamikie mipaka au njia kwa njia sasa ni lazima tujipange kuhakikisha changamoto hii inaisha," alisema.

Awali baadhi ya wananchi wenye kero hizo, Rose Livingstone Mkazi wa Sekei alisema amehangaika na kesi yake ya ardhi tangu mwaka 1989 hadi leo hii na hajapewa nakala za hukumu sita ambapo hadi sasa amepata nakala moja tu ya hukumu na ameambiwa atoe sh. milioni 7. 

Mimi sina hiyo sh. milioni 7 na hadi sasa nahangaishwa kuhusu eneo langu lakini mtu ninayepambana naye anauwezo sina jinsi lakini mahakama imetoa amri abomolewe ukuta ule sasa mimi naombeni mnisaidie kuhusu haki yangu," alisema.

Kutokana na hilo, Gambo aliamuru mhusika huyo abomolewe ukuta huo ili mlalamikaji apewe eneo lake pia alitoa rai kwa wananchi wanaotaka kupimiwa ardhi kuungana kwa pamoja kwenye mitaa yao ili waweze kugharamia upimaji wa maeneo yao kwa sh. milioni 1 zitakazowapatia hati miliki za ardhi.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: