Saturday, July 22, 2017

Zanzibar yapokwa uanachama CAF

ad300
Advertisement
Ikiwa ni miezi michache tangu Zanzibar kukubaliwa ombi lake la kuwa mwanachama wa Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF), imepokonywa uanachama huo.

Rais wa CAF Ahmad Ahmad, amesema Zanzibar ambayo ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, haikufaa kukubaliwa kuwa mwanachama wa 55 wa shirikisho hilo Machi, mwaka huu.

"Walipokelewa bila ya kufuatwa kwa sheria za shirikisho ambazo ziko wazi," amesema Ahmad.

Aliongeza kuwa CAF haiwezi kukubalia uanachama wa mashirikisho mawili kutoka kwa taifa moja.

"Ufafanuzi wa maana ya taifa unatoka kwa Muungano wa Afrika (AU) na Umoja wa Mataifa," alisema Ahmad katika mkutano mkuu maalumu wa shirikisho hilo nchini Morocco.

FIFA kwa upande wake ilikataa kuipokea Zanzibar kama mwanachama hata baada ya hatua ya CAF, iliyoidhinishwa na mtangulizi wa Ahmad kwenye nafasi ya uenyekiti, Issa Hayatou.

Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lakini imekuwa ikiendesha shughuli zake za soka kivyake na kuwakilishwa katika mashindano ya soka ya kanda.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: