Wednesday, July 26, 2017

WFP kunufaisha watu 900,000 nchini

ad300
Advertisement
Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), limezindua Mpango Mkakati wa Nchi (CSP) wa Tanzania utakaodumu kwa miaka minne na kusaidia zaidi ya watu 900,000​.

Mpango huo unaendana na Ajenda ya Umoja wa Mataifa wa 2030 ya Maendeleo Endelevu, inayolenga kuondoa umaskini, kupunguza tofauti ya usawa, kukabili mabadiliko ya tabia ya nchi na kuhakikisha kunakuwa na kilimo endelevu na usalama wa chakula.

Hayo yalisemwa jana Dar es Salama na Michael Dunford, Mwakilishi wa Nchi wa WFP Tanzania, ambaye aliongeza kuwa WFP inakusudia kuimarisha uwezo wa kupata soko kwa wakulima wadogowadogo 250,000.

"Utekelezaji wa mpango huu umeanza Julai 1, mwaka huu baada ya kupitishwa na Bodi Tendaji ya WFP," alisema.

​Pia a​
lisema pia programu ya lishe inayohusisha sekta mbalimbali kwa akina mama 185,000 na kutoa msaada wa chakula kwa zaidi ya wakimbizi 300,000 itaendelea ili kuwapa mazingira salama wenye uhitaji hususan wa chakula.

Aliongeza: "​
U​mesanifiwa ili kuwezesha uwekaji mipango wa muda mrefu ili kuunga mkono Mpango waPili wa Msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDAP II) na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Serikali wa Miaka Mitano."

Akizungumzia mpango huo, Brigedia Jenerali Mbaazi Msuya ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Maafa katika Ofisi ya Waziri Mkuu​,​ ​alisema utayarishaji wake unaipa Serikali fursa ya kuchagua maeneo ya kipaumbele.

"Tunapata fursa ya kupanga kipi kianze ambako kwa kushirikiana na washirika wetu, itaweza kupunguza matokeo ya majanga kwa watu walio hatarini ili waweze kujinusuru na kujiletea usalama zaidi wa chakula," alisema.

Mkazo katika kazi za WFP
​,​ umetajwa kulenga dharura na msaada wa chakula
​ ambapo asilimia 85 ya bajeti ya Shirika ya miaka minne ya Dola za Marekani milioni 455.7 imetengwa kusaidia wakimbizi wapatao 310,000 pamoja na jamii za wenyeji kaskazini-magharibi mwa Tanzania.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: