Monday, July 24, 2017

Wapinzani wajipanga kumng'oa Rais Kabila

ad300
Advertisement
Upinzani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo umetangaza mipango na mikakati yake mipya ya kushinikiza kuondoka madarakani kwa Rais Joseph Kabila wa nchi hiyo kwa kutumia migomo na uasi wa kiraia.
 
Taarifa ya kambi ya upinzani nchini humo imeeleza kuwa wapinzani wanaendelea kufanya maandamano na kuhamasisha uasi wa kiraia ili kumshinikiza Rais Kabila aachie ngazi na kuondoka madarakani.

Tangazo hilo linakuja baada ya siku mbili za mazungumzo ya upinzani jijini Kinshasa, kufuatia wasiwasi kuwa Rais Kabila anayetawala taifa hilo tangu mwaka 2001 huenda akaendelea kubakia madarakani na hivyo kukiuka hata makubaliano yaliyofikiwa mwaja jana.

Uchaguzi ulitakiwa kufanyika mwaka huu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa mujibu wa mkataba uliokusudia kuepusha vurugu za kisiasa nchini humo baada ya Rais Kabila kuendelea kubakia madarakani hata baada ya muhula wake wa uongozi kumalizika Disemba mwaka jana.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa, Agosti 20 mwaka huu, upinzani umepanga kufanya maandamano mfululizo katika mji mkuu  Kinshasa na majimbo 25. 
 
Mgogoro wa ndani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo uliibuka baada ya kuahirishwa tarehe ya uchaguzi wa rais na kadhalika sisitiza la Rais Joseph Kabila la kutaka kuendelea kusalia madarakani nchini humo. 
 
Licha ya kutiwa saini makubaliano baina ya wapinzani na serikali juu ya kufanyika uchaguzi wa rais tarehe 31 mwezi Disemba mwaka huu, hata hivyo inaonekana kuwa, uchaguzi huo hautaweza kufanyika katika tarehe iliyopangwa.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: