Friday, September 23, 2016

RC K'njaro apiga marufuku ufugaji holela

ad300
Advertisement


Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Said Mecky Sadick, amepiga marufuku tabia inayofanywa na Wafugaji ya kuhamisha mifugo kutoka kijiji kimoja kwenda kingine na kudai kuwa kufanya hivyo kunaweza kusababisha maambukizi ya magonjwa kwa mifugo.
Sadick alitoa kauli hiyo jana, alipofanya ziara katika Jimbo la Moshi vijijini, na kuongea na Wananchi wa kata ya Mabogini ambapo alisema wafugaji wamekuwa wakihamisha mifugo kutoka kijiji kimoja kwenda kingine na kusambabisa kusambaa kwa magonjwa ya mifugo. 
Alisema pia kuhamishwa kwa mifugo hiyo kumekuwa sababu kubwa ya migogoro ya Wakulima na Wafugaji hivyo ni vyema kila mmoja akafuata sheria na taratibu zilizowekwa kwa kuheshimiana bila kujali kazi ya mwenzake.
“Chanzo cha migogoro ya ardhi ni kuhamishwa kwa mifugo kutoka kijiji kimoja kwenda kingine na kulishwa katika mashamba ya wakulima huku Serikali ya kijiji ikiwafumbia macho.
“Hivyo kuanzia leo napiga marufuku biashara ya kuhamisha mifugo kutoka sehemu moja kwenda nyingine bila kuwa na kibali maalum cha unapota na kule unapoelekea,” alisema Sadick.
Aidha mkuu huyo wa mkoa aliwataka viongozi wa Serikali ya vijiji kuweka mipango ya matumizi ya ardhi kwa kugawa sehemu ya wakulima na wafugaji ambapo itasaidia kupunguza tatizo la migogoro ya wakulima na Wafugaji.
Kwa upande wake Diwani wa kata ya Mabogini, Emmanuel Mzava, alisema kuwa wanakabiliwa na tatizola chakula katika shule za msingi na sekondari zilizopo katika kata hiyobaada ya baadhi ya Wazazi kukataa kuchangia chakula ili Wanafunzi wale chakula cha mchana bure.
Mzava alisema tatizo lingine linaloikabili kata hiyo ni migogoro ya ardhi baina ya wakulima na Wafugaji, ambapo Wafugaji kutoka katika vijiji vya jirani wamekuwa wakileta mifugo yao na kuingiza katika mashamba ya wakulima na kusababisha migogoro ya mara kwa mara.
Kwa upande wa wananchi, waliiomba Serikali kuwagawanyia jimbo hilo baada ya kumlalamikia Mbunge aliyepo sasa Anthony Komu (Chadema), kutowapigania na kuwasemea matatizo yao Bungeni watu wa tambarare na badala yake amekuwa akiwapigania watu wa milimani.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: