Friday, September 23, 2016

Jela miaka 30 kwa kubaka, kuambukiza kisonono

ad300
Advertisement


Mahakama ya wilaya Tarime mkoani Mara, imemhukumu Mashaka Marwa kifungo cha miaka 30 jela, kwa kosa la kumbaka mwanafunzi wa darasa la sita.
Pia imemhukumu amlipe mlalamikaji faini ya sh. milioni 4 akitoka gerezani na kuchapwa viboko sita kwa kosa hilo ambalo lilimfanya amuambukize mwanafunzi huyo wa shule ya msingi Sabasaba ugonjwa wa kisonono.
Akisoma shitaka hilo mbele ya hakimu Amon Kahimba, Mwendesha mashitaka wa Polisi, Mwanri Mrisho, alidai Machi 12, mwaka huu, saa 9 mchana, mlalamikaji alitoka na kwenda kwenye shamba la Babu yake kujisaidia baada ya choo chao kubomoka.
Alidai baada ya kuvua nguo alivamiwa na kukabwa nyingoni na mtuhumiwa huku akimtishia kumuua kwa kumchoma kisu endapo angepiga kelele, kisha kumpiga ngwala na kuanza kumbaka.
Mwanri alidai mtoto huyo alipiga kelele za kuomba msaada kutokana na maumivu aliyoyapata lakini hakukuwa na mtu maeneo ya karibu hivyo mtuhumiwa alimaliza haja yake na kutoroka.
Mwendesha mashitaka huyo aliendelea kueleza kuwa baada ya kitendo hicho, mtoto huyo wa miaka 13 alirudi nyumbani kwa Babu yake (Siongo Marwa) na kumweleza yaliyompata ambapo walirudi mpaka eneo lile na kuona mahindi yamevunjwa kutokana na purukushani.
Alidai Mzee Siongo (Babu wa mtoto), alimchukua mjukuu wake mpaka kituo cha polisi ambapo walipewa PF3 na kwenda hospitali walikofanyiwa uchunguzi wa kitabibu na kuthibitishwa kuwa amebakwa na kuambukizwa ugonjwa wa kisonono.
Mwanri aliiomba mahakama kumpa mtuhumiwa adhabu kali ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia hizo, kwa sababu imemuharibia Mwanafunzi huyo usichana wake na kumwambukiza ugonjwa wa zinaa.
Baada ya maelezo hayo, Mtuhumiwa alijitetea na kudai kuwa ameshitakiwa kutokana na mgogoro wa ardhi na viwanja kati ya Babu wa Mwanafunzi huyo na Mama yake mzazi hivyo kuiomba Mahakama kumsamehe huku akiomba  nakala ya hukumu kwa ajili ya Rufaa.
Akitoa maamuzi ya kesi hiyo, Hakimu wa Mahakama hiyo, Amon Kahimba, alidai ameridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mlalamikaji mahakamani hapo bila shaka yoyote huku upande wa mshtakiwa ukikosa shahidi.
Alidai hawezi kumpa nakala ya hukumu kutokana na kwamba hakuna ushahidi ulioonyesha kuwa kuna migogoro ya ardhi baina ya wazazi ambapo hata mzazi wake, hakufika kutoa ushahidi.
Hakimu huyo alidai kwa viashiria hivyo inaonyesha huenda mtuhumiwa alitaka kujiokoa kwa kutumia kisingizio cha migogoro ya ardhi hivyo anastahili kuhumu kwa mujibu wa sheria.
Upande wa Mlalamikaji ulikuwa na mashahidi 6 akiwemo mwanafunzi huyo, Babu yake aliyeambatanisha fomu ya majibu ya vipimo hospitalini, tabibu aliyemhudumia mlalamikaji na mpelelezaji wa kesi hiyo. 
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: