Thursday, September 22, 2016

Dar, Pwani kukosa maji

ad300
Advertisement


Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani, hususan maeneo yanayopata huduma ya maji safi kutoka Shirika la Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO), yatakosa huduma hiyo kutokana na kuzimwa kwa mitambo ya kuzalisha maji ya Ruvu Juu na Chini.
Akizungumza na Uhuru jana jijini Dar es Salaam, Meneja Uhusiano wa shirika hilo, Everlasting Lyaro, alisema mitambo hiyo iliyoko mkoani Pwani itazimwa kwa wastani wa saa 12 kesho (24/09/2016), kwa ajili ya matengenezo kwenye njia ya umeme.
Everlasting alisema  wamelazimika kuizima mitambo hiyo ili kuruhusu Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), kufanya matengenezo kwenye laini kubwa ya umeme inayotoka Ubungo kwenda kituo cha chake cha  Mlandizi.
Alisema kituo hicho cha umeme kilichoko Mlandizi mkoani Pwani, ndicho kinachotegemewa kunapeleka umeme kwenye mitambo ya maji ya Ruvu juu na Ruvu chini.
“Kutokana na Matengenezo hayo yatakayofanywa na TANESCO kutakuwepo na ukosefu wa huduma ya maji kwa wakazi wa Mlandizi mjini, Ruvu darajani, Vikuruti, Disunyara, Kilangalanga, Janga, Mbagala, na Visiga, mkoani Pwani,” alisema.
Maeneo mengine aliyataja kuwa ni Maili 35, Zogowale, Misugusugu, Tanita, Kibondeni, Kwa Mathias, Nyumbu, Msangani, Kwa Mbonde, Picha ya Ndege, Sofu, Lulanzi, Gogoni, Kibamba, Kibamba Njia Panda, Shule Kibwegere, Mloganzira, Kwembe, Kibamba Hospitali, Kwa Mkinga na Luguruni.
Aidha aliyataja maeneo mengine yatakayoathiriwa na kuzimwa kwa mitambo ya Ruvu juu na chini kuwa ni Mji wa Bagamoyo, vijiji vya Mapinga, Kerege na Mapunga pia Bunju, Boko, Tegeta, Kunduchi, Salasala, Jangwani, Mbezi Beach na Kawe.
“Mlalakuwa, Mwenge, Mikocheni, Msasani, Sinza, Manzese, Mabibo, Kijitonyama, Kinondoni, Oysterbay, Magomeni, Upanga, Kariakoo, City Centre, Ilala, Ubungo Maziwa, Kigogo, Mburahati, Hospitali Ya Rufaa Muhimbili, Buguruni, Changombe, Keko pamoja na Tabata pia kutaarithiwa na matengenezo haya,” alisema.
Kutokana na hatua hiyo, Meneja huyo alisema DAWASCO inawaomba radhi wananchi na kwamba wanapaswa kuhifadhi maji kwa kipindi hiki, ili wasipate shida wakati mitambo hiyo itakapozimwa.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: