Wednesday, January 14, 2015

Kiwanda cha Dangote kukamilika Agosti mwaka huu.

ad300
Advertisement


UJENZI wa Kiwanda cha saruji cha Dangote kimekamilika kwa robo tatu na kinatarajia kuanza kazi ya uzalishaji Agosti, mwaka huu.



Kiwanda hicho kinamilikiwa na mfanyabiashara maarufu nchini Nigeria, Alhaji Aliko Dangote kilichopo eneo la Msijute mkoani Mtwara, kina  ukubwa wa  hekta 2,971 na kitakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 7,500 kwa siku na uzalishaji ukiongeza kwa mwaka watazalisha tani milioni tatu.



Mwakilishi Mkazi wa kampuni hiyo nchini, Esther Kroll alisema hayo alipozungumza na wajumbe wa Bodi ya Shirika la Petroli Tanzania (TPDC), waliotembelea kiwanda hicho wakati wakifanya ziara mkoani hapa na ujionea kazi za ujenzi zivyoendelea katika eneo hilo.



Esther alisema kikubwa hicho ni kikubwa  Afrika ni kati ya viwanda 16  anavyomiliki mfanyabiashara huyo.



Alisema kukamilika kwa kiwanda hicho kinategemea kuajiri wafanyakazi 10,000 ambapo watatoa kipaumbele kwa wananchi wa Mtwara kuchangamkia fursa hiyo na ikionekana nafasi zingine zitakuwa wazi itawalazimua watafute maeneo mengine.



Mwakilishi mkazi huyo alisema wiki mbili zijazo wanatarajia kutangaza nafasi za kazi na watawapata wananchi wa Mtwara watakaokuwa wanaomba kazi kupitia kwa wenyeviti kwani watakuwa wanawafahamu wakazi wao.



Esther alisema kiwanda hicho ni kikubwa hivyo kutakuwa na malori 600 yatakayokuwa yanasambaza saruji nchi nzima, pia watatumia bandari, reli ya kati na TAZARA hivyo, watakuwa na wafanyakazi wengi.



“ Wapo makandarasi 1,200 ambao ni wazawa, Wachina 1,200 na Wahindi 20 wanaofanya kazi ya ujenzi katika kiwanda hiki kwa sasa,”alisema.


Alisema Alhaji Dangote wakati alipokuwa akiweka jiwe la msingi Julai 27, mwaka 2012 aliahidi kutoa sh. milioni 450 kwa vijiji 10 vinavyozunguka eneo hilo kupitia Benki ya CRDB kupitia vikundi vyao vya Vicoba.



Pia, aliahidi kujenga soko la kisasa , kituo cha polisi , hospitali na shule vyote vitajengwa wakati uzalishaji wa kiwanda utakapoanza Agosti, mwaka huu.



Alisema kiwanda hicho kimejipanga kuanza kutoa fedha hizo kwa  vikundi  mwezi ujao  na watatoza riba ndogo.



Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Michael Mwanda, alipongeza kazi kubwa inayofanywa ya ujenzi wa kiwanda na kwamba kitakapokamilika kitakuwa ni mkombozi kwa wananchi wa Mtwara na wananchi wengine.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: