Sunday, April 6, 2014

Jumuia ya Wazazi Temeke yang'ara katika Siku yao

ad300
Advertisement
Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi (W) TemekeSophia Kanega akipanda mti kwenye Hospitali ya Vijbweni.

Sophia Kanega akiwa na moja ya zawadi za Vitenge walovyovitoa juzi.
WAJUMBE wa baraza la Jumuia ya Wazazi (CCM), Wilaya ya Temeke Mkoani Dar es Salaam juzi wameshiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii kwenye maadhimisho ya siku ya jumuia hiyo Kiwilaya.

Katibu wa Jumuia hiyo Suleiman Ndende alisema kwa kawaida siku hiyo huadhimishwa  Aprili 6 ya kila mwaka lakini wao kama Wilaya waliiadhimisha kabla ili waweze kujumuika na wenzao wa mkoa jana.

Akiongoza shughuli hiyo Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi Wilaya ya Temeke Sophia Kanega pamoja na wajumbe wengine walipanda miti ya Kivuli katika Hospitali ya Mbagala na kutoa zawadi mbalimbali ikiwemo sabuni za kufulia kwa wagonjwa waliokuwepo hospitalini hapo.

Pia waliitembelea Shule ya Msingi Mianzini iliyopo katika Manispaa ya Temeke ili kuona matatizo yanayoikabili shule hiyo na jinsi ya kuyatatua kwa kuyafikisha ngazi za juu za Serikali kwa manufaa ya watoto ambao ni taifa la kesho.

Sambamba na hilo pia waliizawadia Hospitali ya Vijibweni mashine mbili za kupimia magonjwa ya Moyo na Sukari kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa huduma hizo Hospitalini hapo.

Sophia alisema wao kama Jumuia ya Wazazi Wilaya ya Temeke wameamua kuwa mfano kwa Wilaya zingine katika utendaji kazi kwa lengo moja la kuisaidia jamii hususan mashuleni na hospitalini kila mara inapopata wasaa wa kufanya hivyo.

Akizungumza baada ya kumaliza shughuli hizo za kijamii, Katibu wa Siasa na uenezi Wilaya ya Temeke Rutami Masunu alisema katika ziara hiyo ameona kero kadhaa ambazo wao kama Viongozi wanatakiwa wazitatue kwa ajili ya Wananchi.

Alisema kuna uhaba wa Madarasa kwenye Shule ya Mianzini, pamoja na eneo katika Hospitali ya Mbagala ambayo inalihitaji kwa ajili ya upanuzi wa hospitali hiyo inayohudumia Wananchi wengi kwa sasa hivyo Serikali sikivu iliyo chini ya Uongozi wa CCM itaendelea kuzitatua.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: