Sunday, April 15, 2018

Kodi kutozwa kwa watumia mitandao ya kijamii

ad300
Advertisement
WAZIRI wa Fedha wa Uganda Matia Kasaija ameliambia Shirika la Habari la Uingereza Reuters kuwa serikali yake inapanga kuwatoza kodi watumiaji wa mitandao ya kijamii kila siku, kuanzia Julai mwaka huu, hatua inayolenga kuisadia serikali kukusanya mapato.
“Tunahitaji fedha za kuisaidia kuimarisha usalama, kuweka miundo mbinu ya umeme na mambo mengine muhimu,” alisema.
Hata hivyo, wanaharakati wamepinga mpango huu kwa kile wanachosema ni mpango wa serikali ya rais Yoweri Museveni kuminya uhuru wa kujieleza.
Watumiaji wanatarajiwa kutozwa Shilingi za Uganda 200 au 100.
Mapema mwezi huu, rais Yoweri Museveni alimwandikia barua Waziri Kasaija na kumwagiza kuja na mbinu za kukusanya fedha kutoka watumiaji wa mitandao ya kijamii.
Museveni ambaye amekuwa akiongoza nchi hiyo kwa zaidi ya miaka 30 sasa amesema Mamilioni ya raia wa Uganda wamekuwa wakitumia mitandao ya kijamii kusambaza habari za uongo.
Hata hivyo, mpango huu hautawaathiri wanaotumia mitandao hiyo kwa ajili ya masuala ya elimu.
Wanasiasa wa upinzani nchini humo wamesema hiyo ni njia ya rais Museveni kuonesha kuwa anaogopa ushawishi wa mitandao ya kijamii kama Facebook na Twitter.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: