Tuesday, February 6, 2018

Mazungumzo ya amani kuhusu Sudan Kusini yafanyika

ad300
Advertisement
Jumuiya ya Maendeleo ya Serikali ya Nchi za Afrika Mashariki IGAD kwa mara nyingine imeanzisha mazungumzo ya amani kuhusu Sudan Kusini jana huko Addis Ababa, mji mkuu wa Ethiopia, ambayo yametishia kuchukua hatua za kuadhibu pande mbalimbali zinazopambana. 

Mkutano huo unaoitwa Kipindi cha pili cha Baraza la ngazi ya juu la ustawi umefanyika baada ya kusainiwa kwa Makubaliano ya kusitisha mapambano Desemba 24 mwaka 2017, ambayo yalivunjika saa chache baada ya kuanza utekelezaji wake.

Mjumbe maalumu wa IGAD kwenye suala la Sudan Kusini, Ismael Wais amezitaka pande mbili zinazopambana zisitishe mapambano ili kuweka na kuimarisha mafanikio, uaminifu na imani zilizoanzishwa na Makubaliano ya kusitisha mapambano. 

Amesema Umoja wa Afrika, IGAD, Umoja wa Mataifa pamoja na jumuiya ya kimataifa zimetoa taarifa kali za kulaani ukiukwaji wa makubaliano hayo.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: