Tuesday, August 8, 2017

Waziri Maghembe azuru Sao Hill, atoa maagizo

ad300
Advertisement
Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe amewaagiza wadau wa miti wanaotumia misumeno aina ya Ding dong kuacha mara moja kwa sababu haina ufanisi na inapoteza kiasi kikubwa cha magogo.

Alisema umefika wakati wakatumia misumeno ya kisasa ambayo inaufanisi mkubwa kwenye upasuaji mbao na ni rafiki wa rasilimali za misitu ikilinganishwa na iliyokuwa ikitumiwa awali.

Waziri alitoa kauli hiyo mkoani Iringa, alipozuru shamba la miti la Sao Hill na kuzungumza na wadau wa shamba hilo wakiwemo wenye viwanda vya kupasulia mbao.

Katika mkutano wake na wadau hao Aidha, Waziri Maghembe alitangaza kupunguza bei ya  miti aina mikaratusi kuanzia mwaka huu ambapo ada ya tozo za barabara imepunguzwa kutoka shilingi 35,000 hadi shilingi 17,800.

Alisema ameamua kuchukua uamuzi huo mara baada ya kupokea maombi ya wadau wengi kuhusu kupunguza bei ya tozo hizo.

Waziri huyo pia alitumia fursa hiyo kupiga marufuku wanavijiji waojaribu kumega eneo la msitu kwa ajili ya shughuli nyingine kwamba eneo la msitu halimegwi kwa kigezo chochote.

‘’Hakuna kipande chochote cha ardhi katika shamba hili kitakachochukuliwa kwa ajili ya shughuli nje ya hii inayofanyika kwa sasa,’’ alisisitiza Waziri Maghembe.

Aidha alisisitiza vijiji vya jirani la shamba hilo viendelee kupata fedha za mgawo wa miti ili wazitumie kwa shughuli nyingine za maendeleo.

Kwa upande wa Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza, alisema kuwa utaratibu uliotumika mwaka huu wa ugawaji wa malighafi umekuwa mwarobaini wa kupunguza malalamiko kwa wadau ukilinganisha na miaka iliyopita.

Aidha, aliawapongeza wafanyabiashara na wadau wa shamba hilo kwa kulipa kodi stahiki za Serikali.

Kutokana na uamuzi huo wa serikali, wadau hao wa shamba la Sao Hill walisema wameridhishwa na utendaji wa Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe kwenye suala la ugawaji wa malighafi ya miti.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: