Thursday, August 31, 2017

Wajumbe Baraza la Wawakilishi Znz waimwagia sifa TMA

ad300
Advertisement
Ijumaa, Agosti 25, mwaka huu, Kamati ya Ardhi na Mawasiliano wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar ilitembelea Makao Makuu ya Ofisi za Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), yaliyopo jengo la Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam  ili kuona na kupata taarifa mbali mbali zinazofanywa na taasisi hiyo.

Taarifa ya utendaji ya TMA iliwasilishwa na Selemani Selemani (Mchumi), ambaye pamoja na mambo mengine, aliwafahamisha wajumbe wa kamati hiyo kuwa Mamlaka imepokea ‘Certificate of Appreciation’ toka Idara ya Kamisheni ya Kukaliana na Maafa  na Mamlaka ya Usafiri wa Majini (ZMA), kwa kazi nzuri inayofanywa ya kutoa huduma za hali ya hewa katika visiwa vya Unguja na Pemba.

Akizungumza kwa niaba ya wajumbe, Mwenyekiti wa kamati hiyo ya Ardhi na Mawasiliano wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Hamza Hassan Juma, alisifu kazi nzuri inayofanywa na mamlaka katika kutoa huduma za hali ya hewa Zanzibar. 

Mhe. Hamza aliielezea menejiment ya TMA kuwa, huduma za hali ya hewa nchini zinazidi kuimarika hususan kwenye usahihi wa taarifa zinazotolewa kama vile utabiri wa kila siku na tahadhari, hivyo kuongeza imani kwa wananchi katika ufuatiliaji wa taarifa za hali ya hewa ukilinganisha na hapo  awali ambapo jamii ilikuwa na hulka ya kupuuzia taarifa hizo.

Mjumbe mwingine aliyejitambulisha kwa jinala Mhe. Juma, alisema mchango wa TMA unatambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) akitolea mfano wa pongezi zilizotolewa kwa Mamlaka na Makamu wa Pili wa Rais Mhe. Balozi Seif Ali Iddi kwenye Baraza la Wawakilishi la Zanzibar

Kwa upande wa TMA, Mwenyekii wa Bodi ya Ushauri Dk. Buruhani Nyenzi, aliwashukuru wajumbe hao kwa pongezi zilizotolewa na kuahidi kuisaidia Mamlaka kufikia malengo ya juu zaidi katika utoaji huduma kwa kuboresha miundo mbinu. 

Aidha, aliwaeleza wajumbe hivi karibuni alikuwa na ziara ya kutembelea vituo vya hali ya hewa vya Unguja na Pemba ili kujionea hali halisi, hivyo wananchi wategemee huduma bora zaidi kwa kuwa lengo la Mamlaka ni kuongeza na kuviboresha vituo vyake na kuongeza usahihi wa takwimu za hali ya hewa zinazokusanywa.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dk. Agnes Kijazi, aliwashukuru wajumbe na kueleza utendaji kazi wa Mamlaka kwa kuzingatia weledi na ushirikiano uliopo baina ya wafanyakazi wenyewe na wadau wa hali ya hewa.

Alienda mbali zaidi na kusema anajivunia uwepo wa wataalamu wa sayansi ya hali ya hewa wenye sifa za kitaifa na kimataifa ambao mchango wao mkubwa umeonekana katika kuongeza usahihi wa taarifa zitolewazo na TMA katika miaka kadhaa sasa mfululizo.

IMETOLEWA NA MONICA MUTONI, AFISA HABARI WA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: