Saturday, August 12, 2017

TFS kukusanya maduhuli kielektroniki

ad300
Advertisement
Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umeanza kukusanyaji maduhuli kwa njia ya kielektroniki kufuatia marekebisho ya sheria ya fedha ya mwaka 2017.

Pamoja na sheria hiyo, pia umefanya hivyo kutekeleza maagizo ya serikali ya awamu ya tano kupitia kwa Rais Dk. John Magufuli aliyezitaka taasisi za umma kujiunga na mfumo wa kisasa wa ukusanyaji maduhuli. 

Mfumo huo uliotajwa na serikali ni ule uliosanifiwa na Wizara ya Fedha na Mipango ambao unafahamika kwa jina la kitaalamu kama Government electronic Payment Gateaway (GEPG).

Akizungumzia mfumo huo jijini Dar es Salaam, Mhasibu Mkuu wa TFS, Peter Mwakosya, alisema mashamba yote na ofisi za mameneja (DFM's) wa Taasisi hiyo zimeunganishwa katika mfumo huo.
      
Pater alisema kutokana na mazingira ya vizuizi (checkpoints) kutokidhi mahitaji ya mfumo huo hususan kushindwa kuhifadhi vitendea kazi, wakala unaendelea kuunganisha vizuizi vyote kwenye mfumo kwa kutumia vifaa maalumu vinavyoitwa POS.

"Kutokana na changamoto zilizoko kwenye vizuia vyetu, hasa kwenye kukosa miundombinu ya kutunza vifaa muhimu kwa mfumo huu kama kompyuta kwa sasa vizuia vyote tunaviunganisha kwa POS, " alisema. 

Alifafanua kuwa vifaa hivyo vitatumika kukusanya maduhuli na kuhakiki uhalali wa nyaraka zinazokaguliwa katika vituo vyote vya ukaguzi wa mazao ya misitu na nyuki kwa kipindi hiki ambacho vizuizi vinaunganishwa kwenye mfumo wa moja kwa moja.
                  
Pamoja na hayo, alisisitiza maduhuli yote yatakayokusanywa kwenye vizuizi yawasilishwe mapema katika Ofisi za Mameneja wa Misitu wa wilaya ili yaingizwe kwenye mfumo.

"Tuwakumbusha wateja wote wa Mazao ya Misitu na nyuki pia kuzingatia kwamba wanatakiwa kupata hati za madai (Bill) katika mfumo kabla ya kwenda kufanya Malipo, ni muhimu sana," alisema.
                     
Aliongeza pia kwamba wateja hao wa bidhaa za Misitu na nyuki waliokuwa wakitumia stakabadhi zingine kabla ya mfumo huo (ERV), hawataendelea kuzitumia katika vituo vilivyounganishwa na mfumo wa sasa. 

Miezi michache iliyopita, Rais Dk. Magufuli aliagiza taasisi za umma kutumia mifumo ya kisasa kukusanya fedha za serikali ili zisipotee mikononi mwa wajanja wachache agizo lililotekelezwa na TFS kama moja ya taasisi hizo.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: