Sunday, July 16, 2017

MAHAKAMANI KWA KUMUINGIZA MTU MWEUSI KWENYE JENEZA AFRIKA KUSINI

ad300
Advertisement
Willem Oosthuizen na Theo Jackson

Wakulima wawili weupe watafikishwa mahakamani nchini Afrika Kusini , baada ya kutuhumiwa kuwa walimsukuma mtu mmoja mweusi na kumuingiza ndani ya jeneza, huku wakitishia kumwagia mafuta ya petroli na kumteketeza moto, akiwa hai.


Wakati Victor Mlotshwa alipokataa, wakulima hao walimtishia kuwa watamweka ndani ya jeneza hilo pamoja na nyoka.
Victor Mlotshwa
Washtakiwa hao Willem Oosthuizen na Theo Jackson, walikamatwa mwezi Novemba mwaka jana, baada ya video ya kitendo hicho kilipowekwa mitandaoni.
Walisema kuwa, Bwana Mlotshwa alipitia kwenye shamba lao liliko katika jimbo la Mpumalanga, bila ya kuwa na idhini, na walikuwa wakimuadhibu.
Katika kusikizwa kwa kesi hiyo awali, jaji wa mahakama alisema kuwa wakulima hao walikuwa wakatili na waliojaa tabia za ubaguzi wa rangi.

Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: