Sunday, March 18, 2018

Kamati ya Bunge yapongeza utendaji wa TAWA

ad300
Advertisement
Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imezuru mkoani Kagera na kuridhishwa na utendaji kazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) katika Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi na Kimisi (BBK).

Pamoja na mambo mengine, kamati hiyo imetembelea maeneo hayo ili kuangalia kazi za uhifadhi  zinazofanywa, ambapo wameipongeza TAWA kwa kitendo cha kurudisha uasili  wa mapori hayo, hali iliyosababisha kurejea kwa  wanyamapori na uoto wa asili.

Wakizungumza mkoani humo jana, wajumbe wa kamati hiyo ya bunge walisema awali mapori hayo yalikuwa yameharibiwa  kwa kiasi kikubwa kutokana  na  makundi ya mifugo kufanya malisho  katika maeneo hayo.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Nape Nnauye  alisema ameridhishwa  na masuala ya uendeshaji wa mapori hayo huku akiahidi kusaidia serikali kwenye ushauri, ili iweze kuwekeza  miundombinu itakayokuza utalii  katika ukanda wa Ziwa Victoria.

Tunatambua kuwa TAWA ni changa  haijaanzishwa  muda mrefu lakini ndani ya kipindi kifupi  imeweza kufanya  mambo mazuri katika kulinda  Maliasili zetu ,  Sisi  kamati tumeridhisha na utendaji wake,’’ alisema Nape.

Alisema kutokana na utendaji kazi mzuri wa mamlaka hiyo, wataishauri na kuishawishi Serikali iongeze fedha katika  bajeti ya mwaka 2018/2019  ili iweze  kutimiza wajibu yake kikamilifu zaidi.

Kwa upande wake, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla aliielezea kamati hiyo kuwa TAWA ipo mbioni  kubadili mfumo wake katika mapori hayo.

Alisema moja ya mipango, TAWA badala ya kuendelea kufanya shughuli za uwindaji  wa kitalii pekee, imepanga  kuanzisha  utalii wa picha  ili kufungua  fursa za kiuchumi katika ukanda huo.

Waziri huyo alisema  kutokana na mapori hayo kurejea katika uasilia wake baada  kuharibiwa kwa kiasi kikubwa  na uvamizi wa mifugo, hali iliyosababisha wanyamapori  kuhama,   Wizara inafanya utafiti ili kuongeza baadhi ya wanyamapori katika  mapori hayo ili kuweza kuwavutia watalii wengi zaidi. 

Awali kamati hiyo ilipokea taarifa  kutoka kwa Wenyeviti wa Kamati za ulinzi na usalama za wilaya, ambapo miongoni mwa mambo yaliyojitokeza  ni uvamizi  wa  maeneo ya mapori ya akiba kwa kuanzisha shughuli za kilimo pamoja na kulisha mifugo ndani ya hifadhi.

Naye, Mtendaji Mkuu wa TAWA, James Wakibara, alisema  moja ya mikakati ya TAWA ni  kubadilisha aina ya biashara kwa kuanza kuchanganya ambapo TAWA itaendesha  biashara  ya uwindaji wa vitalu pamoja na  utalii wa picha katika mapori hayo kwa lengo la kuiongezea serikali mapato

Alisema Serikali ipo katika mchakato wa kuboresha  miundombinu  kwa kuanza na barabara ndani ya mapori hayo  ili kuweza kuwavutia wawekezaji  kujenga hoteli mbalimbali ambazo watalii watazitumia kwa ajili ya kupumzika.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: