Sunday, September 10, 2017

Wanafunzi wa kike wapewa rai masomo ya sayansi

ad300
Advertisement
Wanafunzi wa kike wa shule za sekondari nchini, wametakiwa kuipinga dhana iliyoenea kwenye jamii kwa kipindi kirefu kuwa masomo ya sayansi ni mahsusi kwa wanaume pekee.

Rai hiyo imetolewa mwishoni mwa wiki iliyopita na wanawake waliofanikiwa kitaaluma kupitia masomo ya sayansi, teknolojia, uhandisi na hesabu katika warsha iliyofanyika kwenye ukumbi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika warsha hiyo, Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Dk. Magreth Mushi, alisema kumekuwa na dhana potofu kuwa masomo ya sayansi yanasomwa zaidi na wanaume kitu ambacho si sahihi.

Dhana kuwa mwanamke akisoma masomo ya sayansi na kufanikiwa huisahau familia kwa sababu ya kutumia muda mwingi kazini ni potofu hivyo umefika muda ipingwe kwa nguvu zote,” alisema Dk. Magreth.

Aliongeza kuwa wakati umefika kwa jamii kuona kuwa mwanamke anaweza kusoma masomo ya sayansi na kufanikwa kufikia ndoto zake ikwemo kuisaidia jamii katika utatuzi wa changamoto mbalimbali.

Sisi kama wanawake tuliofanikiwa tumeliona hili na ndiyo maana tumewakutanisha wanafunzi na wataalamu wanawake waliofanikiwa kupitia sayansi ambao pia wamefanikiwa katika kulea familia zao,” alifafanua.

Naye Mhadhiri wa TEHAMA kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Doreen Kaduma, alisema wao kama wataalamu wanawake katika njia ya mafanikio wamepitia mengi hivyo wana uzoefu wa kuwapatia wasichana wanaosoma michepuo ya sayansi ili wathubutu na kujiamini katika masomo yao.

Sisi tuliosoma sayansi tuna mambo ya msingi tunayopaswa kuwapa wasichana wanaochipukia ili waweze kufika hapa tulipo na zaidi ya hapa,” alisema.

Alisema wanawake waliofanikiwa katika sayansi ni mfano kwa Jamii kwani wanapitia changamoto mbalimbali huivyo wanweza kutoa ushuda kwa wasichana wanaochupukia ili kuwajenga kisaikolijia.

Mwanafunzi Nancy Bilinje anayesoma kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya Chang’ombe mchepuo wa sayansi (PCB), alisema ndoto yake ni kuwa daktari bingwa wa kinamama na watoto na anajitahidi ili kufikia ndoto hiyo.

Programu hii itaniwezesha kukaa na wanawake waliokwishafanikiwa ili nami niweze kupata njia sahihi kufikia malengo yangu,” alisema.

Aidha aliwataka wasichana kutokatishwa tamaa na kwa kujiwekea malengo na kutumia vizuri muda kwa kuisomea kwa bidii.

Warsha hiyo ilikuwa na lengo la kuwakutanisha wataalamu wanawake waliofanikiwa kupitia sayansi  na  wanafunzi wa kike wa sekondari wanaosoma michepuo ya sayansi ili kuwaimarisha kimawazo na kuwapa njia sahihi ya kufikia ndoto zao.

Imeandikwa na Vincent Mpepo wa OUT
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: