Wednesday, September 13, 2017

'Asali yenye Nikotin haina madhara kwa binadamu'

ad300
Advertisement
Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) imetoa ripoti ya utafiti wa asali zilizokusanywa zenye chembechembe za nikotini kuwa zimefanyiwa majaribio na  zimedhihirisha kuwa chembechembe  hizo ni chache na hazina uwezo wa  kudhuru mwili wa binadamu.
 
Akizungumza na Vyombo vya habari jijini Dar es Salaam, Meneja Mawasiliano wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, Glory Mziray alisema TFS wamekuwa wakukisanya sampuli kila baada ya miaka miwili  kutoka kwa wafuga nyuki.

Glory alisema sampuli hizo hupelekwa kwenye  Maabara za kimataifa na mara zote  zimekutwa zikiwa na ubora wa hali ya juu unaokidhi masoko yote ya kitaifa na kimataifa.
 
Alizitaja tafiti  mbili zilizofanyika mwaka 2016 kuwa  lengo lake lilikuwa ni kuainisha madhara ya  ufugaji nyuki kwenye maeneo yanayolima Tumbaku na ameyataja maeneo yaliyofanyiwa utafiti huo kuwa  ni mkoa wa Tabora na Kigoma
 
Pia alisema tafiti hizo zimebainisha kuwa kiwango cha nikotini kinachopatikana  kwenye asali iliyochavushwa katika mikoa inayolima Tumbaku ni sawa na nikotini iliyopatikana kwenye asali  ilivyochavushwa na mimea mingine kama vile  nyanya na miombo hivyo kiwango hicho cha nikotini hakina madhara kwa binadamu.
 
Alisema  watumiaji wa asali wamekuwa wakihukumu uwepo wa nikotini   kwenye asali kwa kuangalia rangi ya asali sambamba na uchungu wa asali lakini asali za Tanzania zinatengenezwa kwa mchanganyiko wa maua ya mimea mbalimbali jambo ambalo linathibitishwa si nikotini peke yake ndiyo inasababisha uchungu bali mimea mingine kama vile muarobaini. 
 
Ofisa huyo aliwataka watumiaji wa asali kuendelea kuitumia kwa vile  asali ni chakula cha kiasili kinachotengenezwa kutokana na mchanganyiko wa mimea mbalimbali.
 
Aliongeza kuwa asali ni mchanganyiko uliotokana na maji, Sukari (fruktosi, glukosi, sakrosi) madini pamoja na vitamin.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: