Tuesday, August 29, 2017

Sportpesa yaitunuku Idara ya Habari-MAELEZO Cheti

ad300
Advertisement
Kampuni ya Michezo ya Kubashiri ya Sportpesa, katika kutambua utendaji kazi wa idara ya habari (MAELEZO), leo Agosti 29, imetoa Cheti cha Shukrani kwa Idara hiyo kwa kushiriki vizuri katika ujio wa timu ya soka ya Everton, iliyowasili nchini Julai, mwaka huu.
 
Akizungumza katika makabidhiano hayo Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari , Rodney Thadeus, aliishukuru kampuni hiyo kwa kutambua kazi nzuri ya Idara ya Habari (MAELEZO) kuanzia kuwasili kwa timu hiyo kwa kuweka mazingira mazuri ya waandishi wa habari.
 
Idara ya Habari ilifanya maandalizi na uratibu wa vyombo vya habari kuanzia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, uwanja wa taifa wakati timu ya Everton inafanya mazoezi pamoja na siku mchezo wao dhidi ya Gor Mahia ya Kenya.
 
“Kwa mazingira yale ya wachezaji wakubwa huwa wanahitaji sana usalama kwa hiyo mtu yeyote ambaye anataka kwenda kuchukua habari lazima awe ametambuliwa na Serikali kupitia Idara ya Habari (MAELEZO) na jukumu hilo tulilitekeleza kikamilifu kuhakikisha kwamba hakuna mwandishi ambaye atazuiliwa kuingia uwanjani”, alisema Rodney.
 
Pia alisema kwamba sportpesa wametambua kuwa kuna Idara ya Habari (MAELEZO) na kutambua kwao inaonyesha jinsi gani Idara hii kuanzia kwa Mkurugenzi mkuu, Wakurugenzi wasaidizi pamoja na maofisa wake wanafanya kazi inayotambulika ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.
 
Aidha Rodney alisema tuzo hiyo itakuwa ni chachu ya kuendelea kufanya kazi kwa kasi zaidi katika Idara hiyo ili kazi za Idara ziweze kufahamika zaidi, lakini kubwa zaidi ni kuizungumzia Serikali na kazi zake katika nyanja zote kuanzania kwenye michezo na maeneo mengine ya uchumi, siasa pamoja na biashara.
 
Kwa upande wake Afisa Uhusiano wa kampuni hiyo, Sabrina Msuya, aliishukuru Idara ya Habari (MAELEZO) kwa kazi nzuri wanayoifanya hususani kutoa ushirikiano katika kufanikisha shughuli hiyo ya ujio wa timu ya Everton.
 
“Tunaishukuru Idara ya Habari (MAELEZO) kwa kutupa ushirikiano wenu kufanikisha shughuli nzima ya Everton kuanzia wanakuja, wakati wa mechi mpaka wanaondoka huu ni mwanzo mzuri na tuanomba ushirikaiano wenu katika kuendeleza soka Tanzania," alisema Sabrina.
 
Wakati wa ujio wa timu ya Everton Idara ya Habari (MAELEZO) ikishirikiana na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ili kuhakikisha kila mwandishi anatekeleza majukumu yake ya kihabari licha ya vibali vya waandishi kuisha wakati wake, jambo ambalo liliwezekana.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: