Saturday, August 12, 2017

'Kesi' ya UBER yawaponza madreva taxi wa Airport Dar

ad300
Advertisement
Serikali ina mpango wa kujenga reli ya kisasa ya Standard Gaugeitakayounganisha kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) na maeneo ya katikati ya jiji la Dar es Salaam. 

Lengo limetajwa kuwa ni ili kuongeza fursa ya kuchagua usafiri sahihi wa haraka kwa abiria atakayewasili na ndege kupitia terminal II na terminal III ambayo ujenzi wake unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka ujao. 

Kauli hiyo imetolewa Dar es Salaam jana na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, aliyezuru JNIA na kuzungumza na wafanyabishara wanaofanya shughuli zao kiwanjani hapo wakiwemo madereva wa taxi.

Alisema tayari ameanza mazungumzo na wakandarasi kuona namna ambavyo reli hiyo itajengwa na kukamilika sawa na kukanilika kwa ujenzi wa jengo na miundombinu ya Terminal III ya kiwanja cha Julius Nyerere. 

Waziri Mbarawa aliyasema hayo akijibu malalamiko ya Mwenyekiti wa madereva taxi JNIA, kuhusu kunyong'onyeshwa kibiashara na teknolojia ya UBER, inayofanya shughuli za kubeba abiria kwa bei nafuu zaidi. 

Alisema mbali na usafiri huo unaosambaa kwa kasi nchini hasa kwenye maeneo ya mijini, teknolojia nyingi zaidi kwenye sekta ya uchukuzi na usafirishaji wa abiria mengi zitakuja hivyo kuwataka wawe wabunifu kwenye biashara yao. 

Alisema kutokana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia, hakuna sababu ya kulalamika kama mtu unaendelea kufanya biashara kama zamani kabla ya maendeleo ya teknolojia, zaidi ya kuamua kubadili biashara iwe ya kisasa. 

"Kama mlivyosikia wakati nyie mnalalamika UBER inawanyima biashara, sisi serikali tunaleta treni ya kisasa kwenda katikati ya mji hivyo ili muendelee kuwepo kwenye biashara hii, lazima mbadilike," alisema. 

Pia aliongeza kwa kusema teknolojia inayotumiwa na UBER hapa nchini iko maeneo mbalimbali kwenye nchi zilizoendelea, hivyo si sahihi kwa madereva taxi hapa nchini hususan wa JNIA kukaa na kuomba msaada wa serikali ili kupambana na UBER. 

Awali, Mwenyekiti huyo wa madereva Antipas George, alisema licha ya wao kufanya kila wanaloagizwa na serikali, biashara yao imekuwa nguvu zaidi hasa baada ya UBER kuanza kufanya kazi nchini. 

"Kwetu UBER ni tatizo, wakati mimi napanga bei ya kupeleka mteja mjini kwa Sh. 30,000 kutoka hapa Airport, UBER wanamtoza mteja huyo huyo kwa safari ile ile kwa Sh. 12,000," alilalama. 

Baada ya majibu ya waziri kuhusu hoja yake, madereva hao walishauri serikali itoe maelezo kwa UBER kutumia taxi ambazo zinalipa kodi zote za serikali ili kuwe na usawa kwenye biashara hiyo. 

Katika kiwanja cha Julius Nyerere jumla ya taxi 150 mpaka 200 zinaelezwa kutoa huduma kila siku ambapo kutokana na ujio wa huduma hiyo mpya ya UBER inayoendeshwa kielektroniki, hali ya kibiashara kwa madereva taxi imekuwa mbaya. 

Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: