|  | 
| Advertisement | 
Serikali ina mpango wa kujenga reli ya kisasa ya Standard Gauge, itakayounganisha kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) na maeneo ya katikati ya jiji la Dar es Salaam. 
Lengo
 limetajwa kuwa ni ili kuongeza fursa ya kuchagua usafiri sahihi wa 
haraka kwa abiria atakayewasili na ndege kupitia terminal II na terminal
 III ambayo ujenzi wake unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka ujao. 
Kauli
 hiyo imetolewa Dar es Salaam jana na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, aliyezuru JNIA na kuzungumza na 
wafanyabishara wanaofanya shughuli zao kiwanjani hapo wakiwemo madereva 
wa taxi.
Alisema tayari 
ameanza mazungumzo na wakandarasi kuona namna ambavyo reli hiyo 
itajengwa na kukamilika sawa na kukanilika kwa ujenzi wa jengo na 
miundombinu ya Terminal III ya kiwanja cha Julius Nyerere. 
Waziri
 Mbarawa aliyasema hayo akijibu malalamiko ya Mwenyekiti wa madereva 
taxi JNIA, kuhusu kunyong'onyeshwa kibiashara na teknolojia ya UBER, 
inayofanya shughuli za kubeba abiria kwa bei nafuu zaidi. 
Alisema
 mbali na usafiri huo unaosambaa kwa kasi nchini hasa kwenye maeneo ya 
mijini, teknolojia nyingi zaidi kwenye sekta ya uchukuzi na usafirishaji
 wa abiria mengi zitakuja hivyo kuwataka wawe wabunifu kwenye biashara 
yao. 
Alisema kutokana na
 mabadiliko ya sayansi na teknolojia, hakuna sababu ya kulalamika kama 
mtu unaendelea kufanya biashara kama zamani kabla ya maendeleo ya 
teknolojia, zaidi ya kuamua kubadili biashara iwe ya kisasa. 
"Kama
 mlivyosikia wakati nyie mnalalamika UBER inawanyima biashara, sisi 
serikali tunaleta treni ya kisasa kwenda katikati ya mji hivyo ili 
muendelee kuwepo kwenye biashara hii, lazima mbadilike," alisema. 
Pia
 aliongeza kwa kusema teknolojia inayotumiwa na UBER hapa nchini iko 
maeneo mbalimbali kwenye nchi zilizoendelea, hivyo si sahihi kwa 
madereva taxi hapa nchini hususan wa JNIA kukaa na kuomba msaada wa 
serikali ili kupambana na UBER. 
Awali,
 Mwenyekiti huyo wa madereva Antipas George, alisema licha ya wao 
kufanya kila wanaloagizwa na serikali, biashara yao imekuwa nguvu zaidi 
hasa baada ya UBER kuanza kufanya kazi nchini. 
"Kwetu
 UBER ni tatizo, wakati mimi napanga bei ya kupeleka mteja mjini kwa Sh.
 30,000 kutoka hapa Airport, UBER wanamtoza mteja huyo huyo kwa safari 
ile ile kwa Sh. 12,000," alilalama. 
Baada
 ya majibu ya waziri kuhusu hoja yake, madereva hao walishauri serikali 
itoe maelezo kwa UBER kutumia taxi ambazo zinalipa kodi zote za serikali
 ili kuwe na usawa kwenye biashara hiyo. 
Katika
 kiwanja cha Julius Nyerere jumla ya taxi 150 mpaka 200 zinaelezwa kutoa
 huduma kila siku ambapo kutokana na ujio wa huduma hiyo mpya ya UBER 
inayoendeshwa kielektroniki, hali ya kibiashara kwa madereva taxi 
imekuwa mbaya. 
 

 
 
 
 
 
0 comments: