Sunday, July 30, 2017

Tetesi za usajili Ulaya 2017/2018

ad300
Advertisement
Mshambuliaji wa Barcelona Neymar, 25, amekubali kusaini mkataba wa miaka mitano kujiunga na Paris Saint-Germain na huenda akakamilisha uhamisho wa pauni milioni 197 wiki ijayo. (RMC)

PSG watawapa Barcelona Angel Di Maria, 29, kama sehemu ya mkataba wa kumsajili Neymar, ili kupunguza kodi ya kutengua kifungu cha uhamisho cha mchezaji huyo wa Brazil. (AS)

Iwapo Neymar ataondoka, Barcelona wataamua kuwawinda wachezaji watatu kutoka EPL- Philippe Coutinho, 25, wa Liverpool, Eden Hazard, 26, wa Chelsea, na Delle Alli, 21 wa Tottenham kuziba pengo. (Mirror)
Barcelona wana wasiwasi kuwa bei kubwa ya kumsajili Philippe Coitinho kutoka Liverpool huenda ikawakatisha tamaa. (AS)

Kiungo wa Barcelona Andres Inisesta, 33, amesema ni Neymar pekee anayeweza kuzungumzia kuhusu hatma yake, akisema hadhani kama euro milioni 200-300 zina manufaa yoyote kwa klabu bila Neymar mwenyewe. (Marca)

Monaco wanasisitiza kuwa hawatamuuza Thomas Lemar, 21, licha ya Arsenal kupanda dau la tatu la takriban pauni milioni 45 kumtaka kiungo huyo. (Telegraph) 

Manchester City wanasema kuwa watampatia Sanchez mshahara wa pauni 320,000 kwa wiki
Manchester City watampa Alexis Sanchez, 28, mshahara wa pauni 320,000 kwa wiki akijiunga nao kutoka Arsenal. (Mail)

Kipa wa Manchester City Claudio Bravo amesema Alexis Sanchez atapokelewa kwa mikono miwili akiamua kwenda Etihad. Bravo na Sanchez wote wanachezea timu ya taifa ya Chile. (24 Horas)

Southampton wamedhamiria kutomuuza beki wao Virgil van Dijk, 26, na watamrejesha katika kikosi cha kwanza licha ya kuachwa katika kikosi kilichokwenda mazoezini Ufaransa wiki hii (Telegraph)
West Ham watakataa dau lolote la kumtaka kiungo mshambuliaji wake Manuel Lanzini, 24. (Evening Standard)
Swansea wanakabiliwa na ushindani kutoka Leeds United katika kumsajili Alvaro Negredo, 31, aliyecheza kwa mkopo Middlesbrough msimu uliopita. (Mirror)
Manchester United wamenza mazungumzo ya mkataba mpya na Ander Herera, 27, ili kuzuia Barcelona kumnyatia kiungo huyo. (Express)

Manchester United wamerejea tena katika kumfuatilia winga wa Inter Milan Ivan Perisic, 28, lakini wana wasiwasi huenda wakamkosa kwa kuwa wamepoteza muda mwingi kumfuatilia Gareth Bale, 28, wa Real Madrid. (Independent)

Meneja wa Inter Milan Luciano Spalletti anadhani mkataba wa Ivan Perisic kwenda Old Trafford haupo tena kutokana na kusuasua kwa mazungumzo kati ya Man Utd na Inter hivi karibuni. (Premium Sport)

Gareth Bale atakataa hatua ya Real Madrid kumuuza kwenda Manchester United kwa sababu hana mpango wa kuondoka Madrid. (Times)

Mchezaji kinda kutoka Brazil, Gabriel Martinelli, 16, anafanya majaribio na Manchester United akitarajia kukamilisha uhamisho wake kutoka Ituano. (Manchester Evening News)
Liverpool wameacha kumfuatilia kiungo wa RB Leipzig Naby Keita, 22, na huenda wakarejea tena msimu ujao ambapo inaaminika huenda wakaweza kumsajili kwa pauni milioni 48. (Liverpool Echo)

Liverpool, Arsenal na Tottenham, zote zinamnyatia kiungo wa Barcelona Rafinha msimu huu. (Mundo Deportivo)

Arsenal wanataka kumsajili kiungo Jakub Jankto, 21, kutoka Udinese. (SportItalia)

Chelsea watalazimika kutoa takriban pauni milioni 17.9 kama wanataka kumsajili kiungo wa Inter Milan Antonio Candreva. (Daily Star)

Everton watataka kumsajili kiungo wa Nice, Jean Seri, 26, ambaye pia ananyatiwa na Arsenal, ikiwa watashindwa kumpata Gylfi Sigurdsson, 27, kutoka Swansea. (L'Equipe)

Habari hizi hazijathibitishwa, tutakujuza mara zitakapothibitishwa.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: