Saturday, July 22, 2017

Taifa Stars yafungashiwa virago CHAN

ad300
Advertisement
Timu ya Taifa ya mpira wa miguu (Taifa Stars), imetolewa kwenye michuano ya kutafuta tiketi ya kushiriki kombe la CHAN baada ya kutoka sare tasa kwenye mchezo wa marudiano dhidi ya Amavubi, timu ya taifa ya Rwanda.

Mchezo huo uliokuwa mgumu na muhimu kwa Taifa Stars, ulipigwa kwenye uwanja wa Amahoro jijini Kigali ambapo timu zote zilicheza kwa kujihami huku Amavubi wakionyesha dhahiri nia yao ya kutokufungwa kwenye uwanja wa nyumbani.

Kwa kuwa Stars na Rwanda zilitoka sare ya bao 1-1, mjini Mwanza kwenye uwanja wa CCM Kirumba, Rwanda inasonga mbele kwa goli la ugenini ambao michuano hiyo ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani (CHAN) itapigwa nchini Kenya mwakani.

Taifa Stars ilianza na 

1. Aishi Manula
2. Boniphace Maganga
3. Gadiel Michael
4. Erasto Nyoni
5. Salim Mbonde
6. Himid Mao
7. Simon Msuva
8. Mzamiru Yassin
9. John Bocco
10. Raphael Daudi
11. Shiza Kichuya

Wachezaji wa akiba walikuwa...

12. Said Mohamed 
13. Hassan Kessy 
14. Nurdin Chona
15. Salimin Hoza
16. Said Ndemla 
17. Joseph Mahundi
18. Stamili Mbonde
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: