Monday, October 14, 2013

Wadau wa mpira wa miguu wilayani Lushoto walia na matokeo ya kuvunja moyo ligi ya mkoa.

ad300
Advertisement


Wapenzi wa soka wilayani Lushoto mkoani Tanga wameeleza kusononeshwa na matokeo ya awali ya timu zao mbili zinazowakilisha makao makuu ya wilaya kwenye ligi ya mkoa inayosimamiwa na Chama cha mpira wa miguu mkoa wa Tanga (TRFA).

Timu hizo ni Lushoto Star pamoja na Lushoto shooting ambazo zote mbili zilicheza mchezo wao wa kwanza tarehe kumi ya mwezi huu kwenye viwanja viwili tofauti.

Lushoto Star walikuwa uwanja wa nyumbani (Hazina) wakiwakaribisha Eagle Rangers ya Tanga mjini na kuambulia kipigo cha 3-1 kwenye dakika 90 zilizokuwa za piga ni kupige kila timu ikitaka kuwaridhisha wapenzi wa soka waliohudhuria mtanange huo kwa kuonyesha kandanda safi lakini mwisho wa siku waswahili walisema ‘mpira magoli’, wageni waliondoka na ushindi huo mnono.

Huko Muheza nako, Timu ya halmashauri ya Muheza iliwakaribisha wawakilishi wengine wa wilaya ya Lushoto, timu ya Lushoto Shooting na bila hiyana wakawachabanga bao 3-0 na kujihakikishia nafasi nzuri mara watakapo rudiana kwenye mzunguko wa pili wa ligi kwenye mechi itakayochezwa mjini Lushoto.

Matokeo hayo yamechukuliwa kwa mtizamo tofauti na wadau wa soka wilayani hapa, kwani walitegemea matokeo mazuri zaidi toka kwa timu zote mbili kutokana na jinsi wanavyozijua timu hizo na mpira wanaoucheza.

Akiongea na willyshechambo blog mmoja wa wadau hao Bw. Pius Kinyashi amesema:

Lushoto bado ina safari ndefu sana kutoka kwenye kandanda, yaani wenzetu huwa hawafanyi kosa kwenye mechi za ufunguzi kabisa. Sasa kwa jinsi matokeo yalivyo kwa timu zote mbili, hali ni ngumu sana mzunguko wa pili, japokuwa mpira hautabiriki lakini bwana mi nazijua hizi timu za Tanga mjini wana defence sana wakijua walishinda round ya kwanza ili wapate hata sare ya bila kufungana.


Aidha mchezaji wa Lushoto Star anayechezea nafasi ya kiungo John Godfrey amesema wamejifunza kutokana na makosa, wamekubaliana na matokeo wanaangalia mechi zijazo.

Tumefungwa tena nyumbani ni aibu hasa kwa mechi ya kwanza, ila Coach katuelekeza wapi tumekosea hivyo tunamuomba tu Mungu game zijazo tufanye poa, ni hayo tu.


Timu zote zinaendelea na mazoezi kwenye uwanja wao wa nyumbani uliopo mjini Lushoto kwa ajili ya kuzivaa timu zingine zilizokuwa kwenye kundi moja kama ilivyopangwa na TRFA kwenye ratiba ya michuano hiyo, ambapo Star watamenyana na KYDC ya Korogwe tarehe15 Oktoba mjini Lushoto, wakati Lushoto Shooting watafunga safari siku hiyo hiyo mpaka uwanja wa Mkwakwani kuunguza nyasi za dimba lile watakapokaribishwa na African Sports ya Tanga mjini
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: